![]() | ||
Raisi Barrak Obama |
Hatua ya Marekani na washirika kulaumu Urusi kwa hatua yake hii imenishangaza na kunisikitisa sana na haikuwa na uhalali wakuitoa kwani wao ndio wavunjifu wakubwa wa sheria za kimataifa na pamoja na haki za binadamu kwani imeshuhudiwa kila kukicha ikiuwa watu katika nchi mbalimbali kama vile Afghanistan,Pakistan,Iraq na hata Syria.
Inashangaza kuona Marekani ikikosoa Urusi huku majesshi yake yakiendelea kuua wanawake na watoto wasio na hatia.Marekani iliivamia Iraq mwaka 2003 bila ya idhini ya Umoja wa mataifa kwa madai ya kuwa inamiliki siliha za nyukilia na kufanikiwa kumuondoa madarakani Raisi wa zamani wa nchi hiyo Saadam Husein.Licha ya kufanikiwa kuingia Iraq bado hadi leo imeshindwa kuthibisha madai hayo.
Pia ili shirikiana na waasi wa Libya kumuondoa madarakani kiongozi wa nchi hiyo Kanali Muammar Gadaf na sasa imepeleka baadhi ya maofisa wake wa kijeshi kutoa mafunzo ya kivita kwa waasi wa Syria wanaopigana kutaka kumuondoa madarakani Raisi Bashir Al-assad.Inafahamika waazi yote Marekani inayafanya haya kwa lengo la kupata maslahai hususa ya mafuta na gesi yaliyopo katika nchi hizo.
Inafahamika wazi kuwa Urusi in masrahi makubwa katika nchi ya Ukraine kutokana na nchi hiyo kuwa na inanunua mafuta na gesi kutoka kwake pia ina ushirikiano mkubwa wa kibiashara yeye vilevile zaidi ya asilimia 90 ya mabomba ya kuuzia mafuta na gesi ya Urusi kwenda Ulaya ya Magharibi yanapitia katika nchi hii ya Ukraine lakini maslahi haya yote yalikuwepo wakati wa utawala wa zamani Victor Youxshenko.
Kwa hiyo hali yoyote ile kuondolewa kwake madarakani kutabadilisha hali ya mambo na ndio maana Urusi imeamua kuingia kijeshi ili kuyalinda kinguvu na hatua siajabu kwa mataifa yenye nguvu kuyavamia kijeshi mataifa madogo.Hivyo kitendo cha Marekani na washirika wake kuilaumu Urusi kwa hatua hiyo haina uhalali kwani nao wanafanya hivohivo katika nchi nyingine hususani za Mashariki ya kati na Afrika Kaskazini.
in