Monday, 14 April 2014

MZEE GURUMO HATASAHAULIKA NA WATANZANIA

Mzee Gurumo akiimba wakati wa uhai wake.
April 13, ni siku isiyosahaulika na watanzania wengi hususa wale wa tathnia ya muziki wa Dansi na hii ni baada ya kumpoteza nguli wa muziki huo nae simwingine bali ni marehemu Muhidini Gurumo ambaye alifariki asubuhi ya jana katika hospitali ya taifa ya Muhimbili.

Gurumo alifariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu hali iliyomfanya astaafu shughuli za muziki mapema mwaka jana na anatarajiwa kuzikwa leo saa saba mchana kijijini kwao alikozaliwa mipango ya maziko inafanyika nyumbani kwa marehemu Tabata Makuburi jijini Dar es salaam.

Gurumo alizaliwa mwaka 1940 katika kijiji cha Msaki,Kisalawe Mkoani Pwani alianza kujishugulisha katika muziki wa Dansi mwanzoni mwa miaka ya sitini,ameimbia katika bendi mbalimbali hapa nchini zikiwemo DDC Mlimani Park,Bima na Msondo Ngoma Music Band.Pia mwanzilishi wa mtindo wa msondo.

Katika uhai wake marehemu alitoa mchango mkubwa katika tathnia hii kwa kutunga nyimbo mbalimbali kama vile Namshukuru Mjomba.Pia alikuwa akihariri nyimbo mbalimbali za Msondo zilizokuwa zikutungwa na wasanii mbalimbali wa bendi hiyo kama TX Moshi,Othmani Momba na wengi neo.


Tuesday, 1 April 2014

ZOEZI LA KUSAFISHA JIJI LINGEANZIA KATIKA HATUA YA KUZIBUA MITARO

Eneo la Kariakoo Jijini Dar es salaam
Kwa zaidi ya siku ya pili sasa katika Jiji la Dar es salaam kumeshuhudiwa operesheni ya kuwaondoa watu wanaofanya biashara katika maeneo yasio rasmi kama vile katika sehemu za kandokando ya barabara na  kwenye maeneo ya viwanja vya wazi kama vile katika viwanja za Zakhiem na mengineyo.

Licha ya operesheni hii kuwa na uhalali wa kisheria lakini imeonekana kuwa ni mwiba mchungu kwa wafanya biashara hao pamoja wateja wao na kusababisha malalamiko kutoka kila kona kutokana na kuona kama wao wanaonewa na Serikali yao.Hii inatokana na udhaifu mkubwa uliofanywa na Jiji wakuwaachia wao kufanya biashara  kwa muda mrefu bila ya kuchukulia hatua kyasi kuwafanya  wajione kama wapo kisheria katika maeneo hayo.

Wahusika waoperesheni hii wamedai kuwa zoezi hili linalenga kusafisha Jiji ili liwe katika mazingira ya usafi pamoja na kurudishwa maeneo ambayo yakitumika kama vile katika stendi za darara na viwanja vya wazi ili yatumike katika shughuli zake kama ilivyo kusudiwa.

Napenda kuwakumbusha watu wa halmashauri ya Jiji kuwa zoezi linaloendelea linaloitwa la kusafisha Jiji lilipaswa kuanzia katika hatua ya kuzibua mitaro ya maji iliyojazana uchafu hadi kushindwa kutiririsha maji kama ilivyo kusudiwa na kusababisha harufu mbaya kwa wakazi wa maeneo hayo na hata wapita njia.

Mitaro mingi iliyopo Dar es salaam hususa katika maeneo ya katikati ya Jiji haifanyi kazi kutokana na kujaa uchafu uliokithiri hatua ambayo inaweza kusababisha magonjwa ya mlipukuko kama vile kipindupindu hususa katika kipindi kama hiki cha majira ya mvua ambayo husababisha kujaa maji kwa mitaro hiyo na kufuluma hadi katika maeneo ya makazi ya watu.

Kwangu mimi binafsi suala la kuzibua mitaro ya maji ni la muhimu zaidi kuliko kuwa ondoa wafanya biashara kwani suala la afya ya binadamu ni la msingi zaidi kuliko kitu kingine. Vilevile kui
acha mitaro hiyo ikitoa harufu mbaya ni aibu kwa taifa ikizingatiwa Jiji la Dar es salaam ndio sehemu penye ofisi nyeti hapa nchini kama Ikulu na wizara mbalimbali.

Pia ndani ya Dar es saalam kuna ofisi mbalimbali za kimataifa kama ofisi za kidiplomasia hali inayo sababisha uingiaji mkubwa wa wageni kutoka nje ya nchi.Hivyo ni vyema halimashauri ya Jiji ingeanza na zoezi hili kwanza ili kuweka afya za Watanzania katika mazingira salama, pamoja na kuliweka Jiji katika taswira nzuri kwetu na hata kwa wageni waingiao hapa nchini

Monday, 31 March 2014

MAREKANI HAINA UHALALI WA KUIKOSOA URUSI

Ni takribani zaidi ya mwezi mmoja sasa dunia imekuwa kwenye mvutano mkubwa kufuatia mzozo wa mataifa makubwa kati ya Marekani na washirika wake dhidi ya Urusi kufuatia hatua ya Urusi kuingia kijeshi mashariki mwa Ukraine katika Jimbo la Crimea kwa kile ilichodai ni kulinda maslahi yake yaliyopo ndani ya nchi hiyo.

Raisi Barrak Obama

Hatua hiyo ya Urusi ilpingwa vikali na Marekani pamoja na washirika wake Uingereza,Ujerumani na Ufaransa kwa madai yakua hatua hiyo ni kuingilia mambo ya ndani ya taifa hilo la Ukraine na ni kinyume cha sheria za kimataifa pamoja na haki za binadamu.

Hatua ya Marekani na washirika kulaumu Urusi kwa hatua yake hii imenishangaza na kunisikitisa sana na haikuwa na uhalali wakuitoa kwani wao ndio wavunjifu wakubwa wa sheria za kimataifa na pamoja na haki za binadamu kwani imeshuhudiwa kila kukicha ikiuwa watu katika nchi mbalimbali kama vile Afghanistan,Pakistan,Iraq na hata Syria.

Inashangaza kuona Marekani ikikosoa Urusi huku majesshi yake yakiendelea kuua wanawake na watoto wasio na hatia.Marekani iliivamia Iraq mwaka 2003 bila ya idhini ya Umoja wa mataifa kwa madai ya kuwa inamiliki siliha za nyukilia na kufanikiwa kumuondoa madarakani Raisi wa zamani wa nchi hiyo Saadam Husein.Licha ya kufanikiwa kuingia Iraq bado hadi leo imeshindwa kuthibisha madai hayo.

Pia ili shirikiana na waasi wa Libya kumuondoa madarakani kiongozi wa nchi hiyo Kanali Muammar Gadaf na sasa imepeleka baadhi ya maofisa wake wa kijeshi kutoa mafunzo ya kivita kwa waasi wa Syria wanaopigana kutaka kumuondoa madarakani Raisi Bashir Al-assad.Inafahamika waazi yote Marekani inayafanya haya kwa lengo la kupata maslahai hususa ya mafuta na gesi yaliyopo katika nchi hizo.

Inafahamika wazi kuwa Urusi in masrahi makubwa katika nchi ya Ukraine kutokana na nchi hiyo kuwa na inanunua mafuta na gesi kutoka kwake pia ina ushirikiano mkubwa wa kibiashara yeye vilevile zaidi ya asilimia 90 ya mabomba ya kuuzia mafuta na gesi ya Urusi kwenda Ulaya ya Magharibi yanapitia katika nchi hii ya Ukraine lakini maslahi haya yote yalikuwepo wakati wa utawala wa zamani Victor Youxshenko.

Kwa hiyo hali yoyote ile kuondolewa kwake madarakani kutabadilisha hali ya mambo na ndio maana Urusi imeamua kuingia kijeshi ili kuyalinda kinguvu na hatua siajabu kwa mataifa yenye nguvu kuyavamia kijeshi mataifa madogo.Hivyo kitendo cha Marekani na washirika wake kuilaumu Urusi kwa hatua hiyo haina uhalali kwani nao wanafanya hivohivo katika nchi nyingine hususani za Mashariki ya kati na Afrika Kaskazini.



























in

Thursday, 27 March 2014

WAKAZI WA MABONDENI ANZENI KUCHUKUA HATUA

Jana na leo kumeanza kushuhudiwa mvua kubwa katika jiji la Dar es salaam na maeneo mengine hapa nchini ambapo kwa mujibu wa mamlaka ya hali ya hewa hapa nchini wamezitaja kuwa ni mwanzo wa mvua za masika na zitaendelea kunyesha mpaka mwezi ujao.

Akizungumza na Shirka la utangazaji Tanzania (TBC), Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Dk.Agnes Kijazi amesema kuwa mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini ni mvua za masika na zitaendelea kunyesha kwa wingi katiaka kipindi chote cha mwezi huu na mwezi ujao.

Kufuatia taarifa hiyo kutoka kwa Mamlaka ya hali ya hewa inayoeleza kuwepo kwa mvua nyingi hapa nchini katika kipindi hiki naomba nichukue nafasi hii kuwaomba ndugu zangu wale wanaoishi maeneo ya mabondeni kuweza kuhama kabla ya madhara kutokea.

Kila mwaka kumekuwa na madhara makubwa ambayo yanatokea kwa wakazi waishio mabondeni pindi zinyeshapo mvua.Hivyo ni vyema watu wakaanza kuchuka tahadhari mapema ili kuepusha madhara na gharama kubwa ya kuhudumiwa kutoka serikalini.

Licha ya madai yenu ya kusema hamna mahali pakwenda pindi mukiondoka katika maeneo yenu mulioyazoea na hata maeneo muliyopangiwa na serikali kama vile mabwepande kuwa ni mbali na mno na maeneo ya kati ya mji amboyo ndio hutumika kufanyia shughuli mbalimbali za maisha kimsingi bado nataka kusisitiza kuwa bado madhara ya mafuriko ni makubwa kwani yanaweza kugharimu maisha ya watu hususani kina mama na watoto ambao ndio huwa wahanga wakubwa wajanga pindi yatokeapo.